KUAZIMU MOYONI DANIELI 1:8
Katika kitabu cha Danieli katika Biblia, tunasoma jinsi Danieli na wenzake walikataa kula chakula cha mfalme Nebukadreza. Walifanya hivyo kwa sababu walitaka kushikamana na Sheria ya Mungu, na kujitenga na unajisi ambayo ilikuwa inaweka masharti ya chakula.
Kulingana na Danieli 1:5-8, Nebukadreza alikuwa ameamuru kuwa watu waliochaguliwa kutoka kati ya wana wa Israeli walelewe na kuletwa kwenye jumba lake la kifalme. Mpango huo ulihusisha kuwapa chakula na divai kutoka kwenye meza ya mfalme mwenyewe. Hata hivyo, chakula hicho kilikuwa ni kinyume na Sheria ya Kiyahudi, kwani kilikuwa kimeandaliwa kwa namna ambayo haikufuata kanuni za kisheria.
Danieli alikuwa mshikamanifu kwa Mungu na alijuwa Mungu ataka nini na kujitolea kwa sheria zake. Alihofia kwamba kula chakula hicho kingekuwa uvunjaji wa amri za Mungu na kujichafua Kwa hiyo, aliamua jaribio la kula chakula cha mboga na kunywa maji badala ya kula chakula kilichopangwa na mfalme. Jaribio hilo lilionyesha matokeo mazuri sana, kwani Danieli na wenzake walikuwa na afya bora zaidi kuliko wengine wote waliokuwa wakila chakula cha mfalme (Danieli 1:15).
Kwa njia hii, Danieli alionyesha uaminifu wake kwa Mungu na kujitolea kwake katika kushikilia maadili yake. Aidha, mfano wa Danieli ulionyesha kwamba mamlaka za binadamu hazipaswi kuwekea mipaka maadili na amri za Mungu. Danieli aliweka Mungu kwanza na alikusudia kwanza kabla ya kutenda na alimtumainia kwa njia yake ya chakula, na Mungu akambariki na kumtunza.
Kwa hiyo, Danieli hakula chakula cha mfalme Nebukadreza kwa sababu alitaka kushikamana na Sheria ya Mungu na kuonyesha nia ya kutojichafua na uaminifu wake kwa Mungu, na Mungu akambariki kwa uamuzi wake huo.
JE TUNAJIFUNZA NINI KUPITIA HABARI HII?
1.KUJUA MUNGU ANASEMA NINI
Tunapojua neno la Mungu linasemaje au mapenzi yake yakoje tunakuwa na wakati bora na sahihi wa kuamua vizuri. Danieli alijua sheria ya Mungu inasemaje. Hivyo basi aliweza kujitenga na kufuata mapenzi ya Bwana wake. Kwa hiyo basi kama mkristo ni lazima kulijua Neno la Mungu ili tuweze kuamua vizuri.
2.KUAZIMU AU KUKUSUDIA KABLA YA KUTENDA
Mambo ya Mungu sana yanahitaji nia kutoka moyoni kuazimu kabla ya kutenda. Danieli alitia nia kwanza kabla ya kukataa kula chakula.
3.KUJITENGA NA UNAJISI
Biblia inatuita sisi watakatifu, ikiwa na maana sisi ni watu tuliotengwa dhidi ya dhambi,ulimwengu na utu wetu wa kale hatunahaja tena ya kujichafua kwa yale ambayo Biblia inasema ni najisi kwetu.
Kwa msaada zaidi๐
Pdickran@gmail.com
0742861404
Prince๐พ

Comments